PRAGMATIKI FULL HAND OUT

                                   PRAGMATIKI

Masamba 2004;anasema pragmatiki ni taaluma ya isimu inayojishughulisha na uchunguzi na uchambuzi wa lugha katika mawasiliano.

Kahili 2019;anasema pragmatiki ina lengo la  umilisi wa kipragmatiki wa maana ya lugha.

                     UMILISI WA KIPRAGMATIKI

 Ni uwezo wa kuelewa maana ya lugha kutokana namuktadha uliopo.Maana ya kipragmatiki hufungamana na muktadha.

Kwa ujumla;Pragmatiki ni taaluma ya isimu inayohusika na kuchunguza jinsi muktadha unavyoasili maana.Pia pragmatiki inafafanua matumizi ya lugha ya watu katika Miktadha mbalimbali.

MUKTADHA;Ni mjumuiko wa mambo mbalimbali.Mambo hayo ni kama yafuatayo:-

      1.Anamzungumzia nani?(Msikilizaji)

      2.Wanazungumza wakiwa wapi(Eneo)

      3.Unazungumza na kundi gani?

      4.Wanazungumzia nini? (Mada)

      5.Ni wakati gani?(Wakati/Muda)

      6.Wana lengo gani?(Dhamira)

      7.Mtazamo wao ni upi?

      8.Wapo katika hali gani?

            -Huzuni,Furaha au ucheshi n.k

       

                    DHANA KATIKA PRAGMATIKI

1.VIMANILIZI

 Ni maana inayoibuliwa kutokana na kile kinachosemwa.

Mfano,Nina hisi baridi kimanilizi chake ni                  kuzima feni kama imewashwa.

           Mbu wanaingia kimanilizi chake ni                  kufungamlango.

2.UDHAMILIZI

 Ni maana inayotambuliwa katika muktadha ambapomsemaji hudhani kuwa msikilizaji anatarifa za awali juu ya kile kisemwacho sasa.

Mfano,Mtoto wa Juma anaumwa ambapo                 udhamilizi wake ni Juma kuwa na                   mtoto/Juma ana mtoto.

3.MATENDO UNENI

 Ni matendo yanayotendwa kupitia uneni(Kunena).

Mfano,Nina kuhukumu miaka tisa jela.

            Nina ahidi kukupenda maisha yangu              yote.

                UHUSIANO WA PRAGMATIKI NA 

                                     SEMANTIKI.

1.Matawi yote mawili yanajikita katika kuchunguza maana katika lugha.

-Ili maana za kipragmatiki ziweze kuchunguzwa ni lazima tungo iwe na maana kisemantiki.

2.Uelewakaji wa maana za ziada zinazofafanuliwa katika taaluma ya semantiki huhitaji Muktadha.

                 UTOFAUTI WA PRAGMATIKI NA  

                                      SEMANTIKI.

                              1.Maana.

                              2.Lengo.

                     3.Vipengele vinavyochunguzwa.

 

                                  Mwisho

Toa maoni yako sehemu ya coment maboresho yafanyike

kama unaswali uliza pia your free.......


Please follow our blog

Next Post Previous Post
No Comment
Add Comment
comment url